Wednesday, February 06, 2013

PATASHIKA NGUO KUCHANIKA MALI NA NIGERIA AFCON LEO


Football | Afcon

Durban ready for battle of the birds


NUSU Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Nigeria, Tai Mkubwa na Tai wa Mali inapigwa kwenye Uwanja wa Moses Mabhida mjini Durban leo.
Vijana wa Patrice Carteron wanaingia kwenye mchezo wa leo baada ya kuwatoa wenyeji, Afrika Kusini kwenye Robo Fainali kwa mikwaju ya penalti, wakati vijana wa Stephen Keshi waliwaduwaza Ivory Coast waliokuwa wanapewa nafasi kubwa ya kufika mbali.
Nigeria ndio inapewa nafasi kubwa sasa kutoka mechi hii inayozikutanisha timu zote za Magharibi mwa Afrika kutinga fainali.
Timu hizo zote zilimaliza katika nafasi ya pili kwenye hatua ya makundu.
Mshambuliaji wa Nigeria, Emmanuel Emenike, anaongoza kwa mabao katika mashindano haya akiwa amefunga matatu hadi sasa na anapewa nafasi kubwa ya kuendelea kufunga hadi leo.
Keshi atakuwa na kikosi chake kamili baada ya kurejea kwa Fegor Ogude aliyekosa Robo Fainali kwa kutumikia adhabu ya kadi, lakini anaweza kupanga kikosi kile kile kilichoitoa Ivory Coast.
Lakini Mohamed Sissoko wa Mali na Samba Diakite wako shakani katika mchezo wa leo na wanakabiliwa na changamoto ya kupambana na majeruhi dakika za mwishoni ili wacheze mechi ya leo.
Nahodha wa Mali, Seydou Keita, ambaye amefunga mabao mawili katika Afcon hii, hakubaliani na kwamba kila mmoja anaipa nafasi Nigeria.
"Watu wanaendelea kusema Nigeria watatufunga Jumatano, kwa sababu kocha wao, Stephen Keshi anaifahamu nje ndani timu ya Mali aliyoifundisha awali, lakini hilo si kweli," alisema Keita.
Keshi pia anabebwa na rekodi, kwani Nigeria haijawahi kufungwa na Mali kwenye mashindano haya tangu mwaka 2002.
Nigeria imeifunga Mali mara mbili katika mara nne walizokutana kwenye Afcon tangu 2002, mechi nyingine zikiisha kwa sare ikiwemo ya 0-0 huko Sekondi-Takoradi, Ghana mwaka 2008 timu hizo zilipotana mara ya mwisho.
© supersport.com

kwa neema fm radio 98.2MHz tunaangaza

Saturday, March 17, 2012

RAMADANI SHAULI GABRIEL OCHIANG WAPIMA UZITO KWA AJILI YA MPAMBANO WAO KESHO


Mabondia Ramadhani Shauli wa Tanzania (kushoto) na Gabliel Ochiang wa Kenya wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito, Dar es salaam LEO kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika KESHO katika ukumbi wa friens Coner Manzese.picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Ramadhani Shauli wa Tanzania (kushoto) na Gabliel Ochiang wa Kenya wakitunishiana misuli baada ya kupima uzito, Dar es salaam LEO kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika KESHO katika ukumbi wa friens Coner Manzese. picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia pamoja na viongozi wao wakiwa katika picha ya pamoja. Bondia Ramadhani Shauli akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Gabriel Ochiang wa Kenya kulia picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Spika wa Bunge akutana na ujumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya UtawalaBora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM)


Katibu Mtendaji wa APRM Bi. Rehema Twalibu akitambulisha ujumbe wa wataalam wanaounda timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) kwa mhe. Spika. Ujumbe huo ulifika Bungeni leo kukutana na uongozi wa Bunge kwa lengo la kujadili maswala mbalimbali katika utawala bora
Mwenyekiti wa Bodi ya APRM Tanzania Prof Assa Mlawa akitoa neno la utangulizi mara baada ya ujumbe huo kufika kuonana na Mhe Spika Ofisini kwake leo
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akijibu baadhi ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa na wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) mara baada ya ujumbe huo kukutana na uongozi wa Bunge dar es Salaam leo. Kushoto kwake ni kiongozi wa ujumbe huo Akere Tabeng Muna na kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya APRM Tanzania Prof. Hassa Mlawa
Naibu Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akifafanua jambo mbele ya wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) mara baada ya kukutana nao Ofisi za Bunge Dar es salaam leo. Kulia kwake ni mwenyekiti wa bodi ya APRM Tanzania Prof. Hassa Mlawa na Mhe. Anne Makinda Spika wa Bunge na kushoto ni kaimu katibu wa Bunge Charles Mloka. Ujumbe huo ulifika Bungeni leo kukutana na uongozi wa Bunge kwa lengo la kujadili
Wenyeviti na Makamu wenyeviti wa kamati za Bunge wakisikiliza kwa makini baadhi ya hoja zilizokuwa zikiulizwa na baadhi ya wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) ambao walikutana na uongozi wa Bunge leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya fedha za Umma (PAC) Mhe. John Cheyo akijibu baadhi ya maswali kuhusu usimamizi wa Bunge katika maswala ya fedha za umma kwa wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) ambao walikutana na uongozi wa Bunge leo kujadili masala mbalimbali katika utawala bora
wajumbe wa timu ya kujitathimini katika maswala ya Utawara Bora barani Afrika (Africa Peer Review Mechanism –APRM) wakiwa katika kikao cha pamoja na Spika wa Bunge na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge mara baada ya kukutana nao Ofisi za Bunge Dar es salaam leo.

MUHIMU KUJUA HAYA KABLA YA SIMBA NA MTIBWA KESHO


Kikosi cha timu ya Simba. Na http://mamapipiro.blogspot.com/
SIMBA ya Dar es Salaam, kesho inatarajiwa kuendeleza harakati zake za kuipokonya Yanga ubingwa wa Yanga, itakapokuwa mgeni wa Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Simba ambao wanaongoza ligi hiyo kwa pointi zao 44, wakifuatiwa na Azam yenye pointi 41, wakati Yanga, mabingwa watetezi wana pointi 10, mara ya mwisho ilifungwa na Mtibwa, Machi 22, mwaka 2009, bao la Omar Matuta lakini tangu hapo wamekuwa wakishinda mfululizo.
Simba inayonolewa na Mserbia Milovan Cirkovic, pamoja na kutarajiwa kulinda rekodi yake mbele ya Mtibwa inayofundishwa na Mkenya, Thom Olaba lakini pia inahitaji kuendeleza wimbi la ushindi katika mechi za ugenini, ikitoka kuifunga Polisi mjini Dodoma 1-0.
Kesho, wachezaji wa kigeni wanatarajiwa kuendelea kuonyesha umuhimu ndani ya Simba kwa kuifungia timu hiyo mabao.
Hadi sasa mabao ya Simba katika Ligi Kuu zaidi yamefungwa na Mnyarwanda Patrick Mutesas Mafisango na Mganda Emanuel Arnold Okwi.
REKODI YA SIMBA NA MTIBWA TANGU 2005:
P W D L Gf Ga Pts
Simba SC 12 8 3 1 19 6 27
Mtibwa Sugar 12 1 3 8 6 19 6
Septemba 25, 2011
Simba 1-0 Mtibwa Sugar
Feb 27, 2011
Simba 4-1 Mtibwa Sugar
Sept 29, 2010
Mtibwa Sugar 0-1 Simba
Machi 22, 2009
Mtibwa Sugar 1-0 Simba
Sep 28, 2008
Simba 1-0 Mtibwa Sugar
Apr 21, 2010
Mtibwa Sugar 0-4 Simba
Nov 15, 2009
Simba 3-1 Mtibwa Sugar
Feb 20, 2008
Simba 1-1 Mtibwa Sugar
Okt 7, 2007
Mtibwa Sugar 1-3 Simba
2007: Hazikukutana kwenye Ligi ndogo
Sept 10, 2006
Mtibwa Sugar 1-1 Simba
Apr 9, 2006
Simba 1-1 Mtibwa Sugar
Okt 5, 2005
Simba 2-1 Mtibwa Sugar
Mei 22, 2005
Mtibwa Sugar 0-1 Simba

Friday, March 16, 2012

GALILE VS MASHALI WATAMBIANA KILA MMOJA KUNYAKUA UBINGWA


MABONDIA Selemani Galile na Thomas Mashali wanatarajia kupanda ulingoni Aprili 9 kuwania mkanda wa ubingwa wa Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa Tanzania (TPBO) litakalofanyika katika ukumbi wa Friends Corner, Manzese Dar es Salaam.
Pambano hilo linatarajiwa kuwa kati uzito wa kg 75 raundi 10 likiratibiwa na TPBO.
Wakitambiana Dar es Salaam jana, wakati wa kuonyeshwa mkanda huo Galile alisema atahakikisha anafanya mazoezi ya kutosha ili kuweza kuunyakua mkanda huo kwani anauhakika atauchukua kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao.
"Mkanda lazima niiuchukue kwani najua Mashali haniwezi na hataweza kunifanya nisichukue mkanda hivyo najiamini na mkanda ni wangu," alisema Galile.
Naye kwa upande wake Mashali alisema raundi 10 ndio zitaamua mkanda ni wanani lakini anaimani ataunyakuwa kwani anamazoezi ya kutosha na bado ataendelea kujifua na kuhakikisha anaibuka bingwa.
"Ninauwezo, nimejipanga na ninauhakika nitaunyakua mkanda lakini yote raundi 10 ndio zitaamua nani bingwa," alisema.
Naye kwa upande wake Rais wa TPBO, Yassin Abdalah alisema mkanda huo ulikuwa wazi hivyo wakaamua kuwaambia mapromota ambapo alijitokeza Prospa Rweyomamu ambaye ndio ameandaa pambano hilo hivyo bingwa atakayepatikana ndio utakuwa kwake akisubiri mpinzani
 
Mbali ya kuwepo na mpambano huo siku hiyo kutakuwa na huuzwaji wa DVD za Mafunzo ya Mchezo wa Masumbwi wakiwemo mabondia Lenox Lewis, Evander Holfiled,David Haye, Waldmil Klitichiko,Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roj Jones na wengine wengi

Zitakuwa zikisambazwa kwa ajili ya kuwapa mabondia,mashabiki marefarii kutambua sheria na kanuni za mchezo huo Duniani ambazo zimeandaliwa na Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini, Rajabu Mhamila Super D Alisema kuwa tangia aanze kutoa mafunzo kwa njia hiyo watu wengi wameanza kuwa na uwelewa wa mchezo wa masumbwi nchini kwa kutambua sheria na mambo mbalimbali ya mchezo alisema Super D boxing Coach ambapo mpaka sasa ameweza kutoa matoleo nane tofauti ya mabingwa wa ngumi Duniani Akichanganya na mabondia wa Nchini.